Kuamua kuingia katika biashara ni majumuisho ya utayari wa kisaikolojia, kiakili, kiuchumi na kukabiliana na hatari au vitisho vyote vitakavyojitokeza kwenye biashara
Maeneo manne ni muhimu yapatiwe taarifa halisi na kuchukua hatua ili uweze kumudu kufanya biashara husika
| Mazingira wezeshi | Mazingira pingamizi | |
| Mazingira ya Ndani |
Uwezo Uwezo wako katika kuendesha biashara mfano: utaalam, vitendea kazi, kiwanja nk. |
Udhaifu Udhaifu wako katika kuendesha biashara mfano: ukosefu wa utaalam, vitendea kazi, kiwanja nk. |
| Mazingira ya Nje |
Fursa Kuwepo kwa sera nzuri, katiba nzuri, hali ya hewa nzuri, mwitikio wa jamii nk |
Vitisho Kutokuwepo kwa sera nzuri, katiba nzuri, hali ya hewa nzuri, mwitikio mbaya wa jamii nk |
Baada ya kujua udhaifu wako, pata mafunzo
Mfano:- Ya kupata ufundi au kubadili mitizamo
Kupata utaalam wa kiufundi katika biashara husika
i) Fursa nzuri zilizopo
ii) Vitisho au hatari zitakazoikabili biashara yako (vihatarishi vya biashara husika kama vile sera mbovu, barabara mbovu, hali ya hewa mbovu nk)
i) Kutengeneza bidhaa (Manufacturing)
ii) Kuuza bidhaa (Trading)
iii) Kutoa huduma (Service)
Kutengeneza bidhaa (Manufacturing)
Kutengeneza bidhaa ni kutumia rasilimali watu na malighafi ili kutengeneza bidhaa ya kuuza kwa mlaji au mchuuzi. Bidhaa ni kama vyakula, vyombo, nk
Kuuza bidhaa (Trading)
Kuchuuza bidhaa zilizotengenezwa hapo juu no. A(a)
Kutoa huduma (Service)
Kutumia ujuzi wako au wa wengine katika kuwahudumia watu na shida zao kwa malipo. Mfano kufundisha, kutibu, kusafirisha, kutumbuiza nk
i) Ukubwa wa soko
ii) Mgawanyo wa soko
iii) Aina ya soko/masoko
iv) NK
Fuatilia maelezo ya kila mfumo ukitilia maanani faida na hasara za kila mfumo. Unaweza pia kumtumia mshauri wa masuala ya biashara kukushauri kulingana na mazingira yako utakayofanyia biashara.
i) Mtu mmoja (sole proprietor)
Faida yake
Kuanzisha ni rahisi
Maamuzi hupitishwa kwa haraka kwa hiyo hakuna urasimu
Hasara yake
Biashara ikipata shida mmiliki anahusika na hasara kama vile ya ufilisi nk
ii) Ushirika (>watu wawili) (partnership)
Faida yake
Kuanzisha ni rahisi
Maamuzi hupitishwa kwa haraka kwa hiyo hakuna urasimu
Hasara yake
Biashara ikipata shida wamiliki wanahusika na hasara kama vile ya ufilisi nk
Mikataba inayoingiwa na mmoja wa washirika huwabana na wengine wasiohusika
iii) Kampuni ya umma au mashirika ya umma (public companies)(zaidi ya watu wawili bila kikomo)
Faida yake
Utambulisho wa kisheria
Ukomo wa ufilisi upo kwenye kampuni husika na sio wenye hisa
Ni rahisi kuvutia mitaji mikubwa kupitia masoko ya hisa
Hasara yake
Haina usiri hivyo ni hatari kwani washindani wa biashara husika wanaweza kutumia taarifa hizo kujipanga
Muda na rasilimali muda kupotea kwa shughuli za kihasibu na kazi za makaratasi
iv) Kampuni ya binafsi yenye ukomo wa hisa (private companies limited by shares) (watu wawili hadi 50)
Faida yake
Utambulisho wa kisheria
Ukomo wa ufilisi upo kwenye kampuni husika na sio wenye hisa
Kazi za makaratasi ni chache ukilinganisha na makampuni ya umma
Mlolongo wa taratibu za kisheria ni chache ukilinganisha na makampuni ya umma
Hasara yake
Gharama katika kuanzisha tofauti na biashara binafsi
Huruhusiwi kuuza hisa katika masoko ya hisa
Kampuni li lazima angalau iwe na wakurugenzi, katibu na mhasibu
Ni lazima ifanyiwe ukaguzi wa mahesabu kila mwaka
v) Kampuni ya binafsi yenye ukomo wa udhamini (private companies limited by guarantees) (watu wawili hadi 50)
Faida yake
Utambulisho wa kisheria
Ukomo wa ufilisi upo kwenye kampuni husika na sio wenye hisa
Kazi za makaratasi ni chache ukilinganisha na makampuni ya umma
Mlolongo wa taratibu za kisheria ni chache ukilinganisha na makampuni ya umma
Hasara yake
Gharama katika kuanzisha tofauti na biashara binafsi
Huruhusiwi kuuza hisa katika masoko ya hisa
Kampuni li lazima angalau iwe na wakurugenzi, katibu na mhasibu
Ni lazima ifanyiwe ukaguzi wa mahesabu kila mwaka
vi) Jumuiya (association)
Faida yake
Utambulisho wa kisheria
Inavutia wahisani
Ni ya watu wachache waliokubaliana
Hasara yake
Ukiritimba katika kupitisha maamuzi
Ugomvi wa mara kwa mara
Haina kinga kwa waazilishi
vii) Vyama vya ushirika
Faida yake
Utambulisho wa kisheria
Inavutia wahisani
Ni ya watu wachache waliokubaliana
Hasara yake
Ukiritimba katika kupitisha maamuzi
Ugomvi wa mara kwa mara
Haina kinga kwa waazilishi
viii) Mashirika yasiyo ya kiserikali
Faida yake
Utambulisho wa kisheria
Inavutia wahisani
Ni ya watu wachache waliokubaliana
Hasara yake
Ukiritimba katika kupitisha maamuzi
Ugomvi wa mara kwa mara
Haina kinga kwa waazilishi
i) Kama ni sheli itabidi iwekwe kando ya barabara yenye magari mengi
i) Teknolojia itasaidia kujua
a) Aina ya watumishi
b) Aina ya vitendea kazi mashine /mitambo
Mfano kilimo cha maksai na kukamua kwa mashine
ii) Teknolojia nzuri ni lazima iwe na sifa zifuatazo
a) Ni rahisi kutumiwa
b) Iwe rahisi kupata msaada kama mafundi nk
c) Iwe inaendana na tamaduni husika
d) Iwe ni rafiki wa watu na mazingira
e) Iwe na gharama ndogo za uendeshaji
f) Inaendelezeka
Mashine na mitambo mingine itategemea sana uchaguzi wa teknolojia hapo juu 8(i)
Mashine zote na mitambo ni lazima kuzingatia yaliyotajwa hapo juu 8(ii)
i) Hii hufanywa mara nyingi kwenye manispaa husika. Leseni kwa wafanya biashara ndogondogo ni bure (biashara ndogondogo ni ile ambayo mauzo yake hayazidi Shs 20 milioni kwa mwaka)
Mambo muhimu ya kujua katika kuandika Mchanganuo wa Biashara
Kutafuta mikopo kwa kufuata utaratibu wa taasisi za fedha husika
Taasisi nyingi huhitaji yafuatayo
Hii ifanywe ili mwenye biashara apate ufahamu wa kiufundi juu ya biashara yake hasa kutoka kwa taasisi husika au mshauri wa biashara (consultant).
Kama ni umeme hakikisha iko sawa na umeme utakidhi matakwa ya biashara.
Kama ni mafuta uhakikishe mafuta inapatikana na bei haitaadhiri bei ya bidhaa
Wataalam husika wafanye hii kazi
Wafanyakazi wako wengi mtaani, lakini kumpata mtu atakayekidhi matakwa ya biashara yako kwa maana ya ubora na kufikia lengo la uzalishaji inahitaji usambazaji wa taarifa kwa upana zaidi na kwa maeneo maalum ambayo unategemea wafanyakazi watoke. Mfano vyuoni, makanisani nk
Unashauriwa pia kutumia marafiki na ndugu wa karibu ili upate mfanyakazi ambaye ni bora zaidi
Malighafi bila ubishi ni kiungo muhimu kwa biashara yeyote inayohusisha bidhaa. Vyanzo vya kupata malighafi ni muhimu ijulikane na iwe ya uhakika.
i) Uzalishaji wa majaribio , Kuuza kwa majaribio kutoa huduma kwa majaribio muda – miezi 2-6, nk
ii) Kuanza biashara rasmi
i) Kutunza siri ya unavyozalisha au kutoa huduma tofauti na wengine
ii) Tunza vizuri siri zingine za biashara yako
i) Epuka majengo ambayo ni rahisi kuwaka moto, kubomolewa na wezi, wizi katika pesa za mauzo, utapeli wa bidhaa katika kununua na kuuza nk.
- Kufikia wateja (fikiria utamfikiaje mteja wako wa kwanza – maelezo zaidi yatakuwepo katika mchanganuo wa biashara)
- Kusambasa huduma/bidhaa
- Kuweka bei
- Kutangazia biashara
- Promosheni nk.
- Hii ifanywe kila mara ili kujua kama wateja wamebadilika au bado Ili kujua kama wanapenda huduma/bidhaa zako au la.
- Kujua biashara yako imekamata asilimia gani katika soko
- Kupata maoni ya wateja ili kuboresha biashara/huduma/bidhaa
Namna ya kufanya utafiti
i) Utafiti wa kuendelea
Kila mteja anaponunua bidhaa, ajaze fomu maalum ya maoni. Mfano ya jinsi alivyohudumiwa, bei ya bidhaa, usindikaji, ubora nk
ii) Utafiti maalum
Huu ufanywe wakati wa kutoa vivutiuo maalum au promosheni maalum.
Mteja wa promosheni ajaze fomu maalum ya maoni. Mfano ya jinsi alivyohudumiwa, bei ya bidhaa, usindikaji, ubora nk
Hii ni kuhakikisha kuwa biashara inakwenda kama ilivyobuniwa /pangwa.
Hii ni kujua kama biashara imekwenda kama ilivyobuniwa /pangwa.
Mambo ya kuangalia
Unaweza kumuajiri au kumtumia mtaalam wa sekta hiyo kufanya taadhmini ya biashara yako.
Fanya sawa sawa na matokeo ya tathmini/utafiti
Nawashukuru sana kwa utaalaam huu juu ya ujasiriamali.Kazi yenu ni njema sana.