Njia 7 za kupata mtaji wa biashara

Njia 7 za Kupata Mtaji wa Biashara

Njia za kupata Mtaji wa biashara: Baada ya kuamua kuingia kwenye biashara/ ujasiriamali, sasa unahitaji mtaji wakufanyia na kukuzia biashara yako.

Mambo muhimu kuyajua:

Sio kila biashara inahitaji mtaji au mtaji mkubwa!

Kuna biashara zingine unahitaji tu kufahamiana na watoa bidhaa au huduma basi. Mfano biashara ya bodaboda, unahitaji tu kufahamiana na mwenye boda boda wewe unafanya kazi kwanza halafu unapeleka sehemu ya makubaliano yako na tajiri baadaye

Hata kama biashara yako itahitaji mtaji mkubwa unaweza siku zote funja funja hayo malengo ya biashara katika ngazi ambayo unaweza anza na mtaji unaoweza kumudu kuupata.

Mfano unaweza kuwa unataka kuwa na hoteli kubwa ya biashara. Hapa unaweza anza na mgahawa na baadaye ikakua

Mfano wa pili

Labda unataka kuwa na supermarket, unaweza anza na mtaji wa 10,000 kuunza vitunguu, chumvi kwa nyumba za jirani mpaka ufukishe mwaka utakuwa na mtaji mkubwa ajabu.

Kama biashara yako itahitaji mtaji kwanza fikiria mambo manne (4) yafuatayo

  1. Aina ya biashara (Kuzalisha, kuchuuza, huduma)
  2. Aina ya soko (kipato kidogo, wanawake tu, wanaume tu, watoto tu, vijana tu, kijiji au mtaa tu nk)
  3. Ukubwa wa mtaji (Mdogo, wa kati au mkubwa?)
  4. Ufahamu wako kwenye biashara yako – Elimu/Ujuzi nk

Majibu ya maswali hapo juu ndio itakayoamua wewe upate mtaji wapi

Sasa swali, wapi utapata huo mtaji nk.

Mlolongo huu hapa chini utakusaidia kujua ni wapi utapata huo mtaji wa biashara.

1. Mali Binafsi

Kama una shamba, fedha, nyumba, gari, mifugo, mazao nk unaweza kutumia mali hizi kama mtaji wa biashara

Kumb. Ukishakubali kuwa mfanyabiashara wewe utakuwa daima ni mtu wa kununua na kuuza. Kwa hiyo hata kitanda chako unachokipenda sana kwa wakati fulani unaweza lazimika ukiuze ili upate mtaji wa biashara. Muhimu usiingie kichwa kichwa kwenye biashara na kujiletea hasara.

Faida: Haina riba, hata ikitokea bahati biashara ikafilisika haiwezi filisi na mali zingine kwani hakuna dhamana ya mali yako.

Hasara: Hakuna msukumo wa biashara kwani mhusika hajali hata akipata hasara, Hivyo ni vigumu kupata faida na biashara kukua.

2. Wabia wa Biashara

Saa nyingine unatakiwa kuwatumia watu wengine ili kupata yafuatayo

  1. Mtaji wa mali
  2. Mtaji wa mawazo na fikra tofauti

Wabia wa baishara yako inaweza ongeza kasi ya kukua kwa biashara kwani fikra tofauti inaweza kuwa chachu ya maendeleo ya biashara husika ukiachilia mbali mtaji ambao wabia wako watakuja nao.

Inabidi lakini uwachague kwa uangalifu mkubwa wabia wako kwani wengine wanaweza kuwa ni wavurugaji na sio wa kuaminiwa.

Faida: Kuongezeka kwa kasi ya kukua kwa biashara kwa sababu ya fikra tofauti

Hasara: Mifarakano yenye kuweza kuua biashara ni dhahiri

3. Wawekezaji wa Biashara

Wawekezaji ni watu ambao wanaweza toa mali na pesa zao kukuwezesha wewe kufanya biashara yako lakini wao watahitaji baada ya muda wa uwekezaji warudishiwe pesa au mali zao na riba mliokubaliana kwenye mktaba wa uwekezaji.

Faida: Uhakika wa mtaji na hivyo uhakika wa kufanya biashara

Hasara: Biashara isipotengeneza faida kwa muda mliokubaliana inaweza sababisha kushitakiana na hatimaye biashara na mali zako kufilisiwa

4. Mkopo Kutoka kwa Watu wa Karibu

Ndugu/jamaa/marafiki na majirani wanaweza kuwa ni chanzo kizuri ya mtaji usio nariba.

Wanaweza kukupa fedha taslimu, wanyama, vitu kama mashine, mitambo, nyumba, ardhi, gari, kompyuta, na vifaa mbalimbali

Faida: Ni rahisi kupata mkopo bila mlolongo wa masharti, uwezekano wa kufilisiwa ni mdogo au hakuna kabisa

Hasara: Kwa vile ni mkopo wa ndugu/jamaa, jirani na marafiki, hakuna msukumo wa kufanya biashara kwa sababu hakuna kufilisiwa hivyo ni ngumu kupata faida na pia kukua kwa biashara yako

5. Mkopo Kutoka Kwenye Vyama, Vikundi nk

Vyama vya kijamii, kitaaluma, vikundi vya kuweka na kukopa, Vikoba vinaweza kuwa chanzo cha karibu kupata mkopo wa biashara wenye riba na masharti nafuu. Unachotakiwa tu ni kuwa mwanachama wa chama chenye kukopesha na kufuata masharti ya chama husika.

Faida: Uhakika wa mtaji japo unaaza na mdogo, uanweza kuepuka kufilisiwa mali zako. Kunakuweo na msukumo kwa kiwango fulani ya kufanya biashara na hivyo uwezekano wa kupata faida na biashara yako kukua

Hasara: Mtaji ni mdogo pale unapooanza

6. Mkopo Kutoka Kwenye Mashirika ya fedha (Micro-Credit Enterprises)

Mashirika kama Pride Tanzania, Vision Tanzania (zamani ikiitwa SEDA), Finca, Faida nk ni hatua nzuri kwa biashara ndogo kwani nao kama ilivyo vikoba wanatoa mikopo midogo kwa masharti nafuu.

Faida: Mlolongo mdogo, dhamana ni rahisi, wanaelimisha

Hasara: Riba ni kubwa, biashara ikifeli utafilisiwa mali ulizoweka dhamana

7. Mkopo kutoka Benki na Tasisi kubwa za Fedha

Mkopo unaohusisha benki ni sharti iwe ni biashara kubwa na mhusika awe na uhakika na soko pamoja na mtaji kurudi.

Mabenki mengine wanatoa mikopo mikubwa na midogo kwa pamoja.

Faida: Uhakika wa kupata mkopo mkubwa, pia msukumo wa kufanya biashara ni mkubwa na hivyo uwezekano mkiubwa wa kutengeneza faida

Hasara: Mlolongo wa kuupata ni mrefu, Kwa bahati mbaya biashara ikifeli, unafilisiwa haraka mali uliyoweka dhamana

Masharti ya mkopo

–          Dhamana kama vile nyumba, arthi, mazao, kikundi n.k.

–          Mchanganuo wa biashara

–          Biashara inayo endelea(<miaka 3)

–          Kuwepo kwa ofisi kama ni mkopo mkubwa zaidi ya milioni 3

–          Biashara iliyosajiliwa kam ni biashara kubwa

–          Riba ya mkopo

–          Kiasi cha mkopo na uwezo wa mkopo

–          Muda wa kurudisha mkopo na riba

Mwisho (End):

Kama umependa makala hii weka maoni yako ya shukrani hapo chini au washirikishe marafiki zako wa kwenye Facebook, Instagram, Linkedin, Whatsapp, Twitter na kwenye email au mitandao mingine ya kijamii. Wasiliana nasi kama unataka kuweka kwenye blogu au website yako kwa maelekezo zaidi

If you found this article helpful please leave the comment below or share to your friends in Facebook, Instagram, Linkedin, Whatsapp, Twitter and in email or other social media. Contact us if you plan to list in your blog or website for further instructions.

Tutembelee kwenye mitandao ya kijamii hapa chini:

We offer but not limited to the following:
Business Office Documents Development, Company Registration, Business Plan Development, Curricula Development for colleges, Office Digitization Consultancy, Online Presence and Marketing Consultancy, Leadership and Management Consultancy, Constitution Development  and much more

English Form

Fomu ya Kiswahili


city, country
mji, nchi